1Wakorintho 5:6-8
“Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima? Basi jisafisheni mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani Kristo”
TAFAKARI
Neno Chachu katika Biblia limetumika kama “mfano”. Sasa waweza kuamua kuwa chachu nzuri ama mbaya. Kwa maana hiyo tunatakiwa kuacha mambo tuliyokuwa tunafanya zamani ya uovu na udhaifu. Tunatakiwa kudumu katika chachu ya uchaji wa moyo uliozungukwa na roho wa kweli. Tujisafishe na tutakate ili kujisifu kwetu kusiharibu ukaribu wetu na yeye.
SALA
Mwenyezi Mungu tunaomba utujalie tuweze kutumika vizuri na kuwa mfano mzuri kwa jamii kwa maana ulimtoa mwanao wa pekee Yesu Kristo awe mkombozi wetu. Tufunulie macho ili tukusifu kwa kila namna itupasavyo tudumu ndani yako daima. Amen.
©IYK-NENO
www.iykcolumbus.org